Header Ads

ad728
  • Breaking News

    UREMBO

     Njia ya Asili ya Kuondoa Mafuta Katika Ngozi Ya Uso Wako

     Njia ya Asili ya Kuondoa Mafuta Katika Ngozi Ya Uso Wako 

    ngozi yenye mafuta huwa kerosana kwa wakina dada  hasa usoni kwa sababu moja ya adhabu ya ngozi yenye mafuta ni kuwa na chunuzi nyingi sana usoni. watu wengi wanaangaika na tatizo hilo na hata kuanza kutumia vipodozi vikali wakati kuna njia rahisi ya asili inaweza kusaidia kuondoa tatizo hilo.

    Ni vizuri kutengeneza mask ya asili kuliko kutumia vile za viwandani ambazo muda mwingie uweza kuwa na kemikali kali sana, mask ya limao na asali imependekezwa kuwa moja ya vitu asili na vya haraka na bei nafuu kuvitumia nyumbani kwa ajili ya urembo wa uso wako.

     mahitaji

    • ute mweupe wa yai
    • vijiko vitatu vya juisi ya limao
    :Changanya juisi ya limao na ute mweupe wa yai kisha paka usoni , kwa muda wa dakika kumi na tano subiri ikauke na kisha nawa uso wako na maji safi na sabuni.
    NB:Mchanganyiko huu ulainisha ngozi ya uso na kuwa laini lakini pia upunguza ukubwa wa matundu ya  ngozi ya uso wako.

    Matumizi ya ndizi katika urembo

    Ndizi

    Ndizi. Picha/MAKTABA 
    Kwa Muhtasari
    Ndizi ni chakula na pia bidhaa muhimu katika urembo.


    Matumizi ya ndizi katika urembo
    KANDO na kulika, ndizi zina manufaa mengine, hasa katika urembo wa ngozi.
    Ndizi zina virutubisho muhimu vinavyoboresha ngozi. Ndizi pia zina aina tatu za sukari zinazojulikana kama ‘sucrose’, ‘fructose’ na ‘glucose’ .
    Hakikisha unanawa uso wako mara tatu kwa siku. Unapofanya hivyo unaondoa uchafu.
    Ndizi pia husaidia kuzuia chunusi.
    Hakikisha unanawa uso kwa sabuni ambayo inaendana na ngozi yako. Ikiwa ngozi yako ni ya mafuta, hakikisha unatumia sabuni ambayo itakuacha ukiwa mkavu na kama ngozi yako ina ukavu, jioshe na sabuni itakayokufanya uwe na unyevu.
    Kulainisha ngozi
    Changanya asali na ndizi moja iliyopondwa na upake kwenye uso na shingo. Nawa uso kwa maji ya fufutende baada ya muda wa nusu saa. Fanya hivi angalau mara moja kwa wiki.
    Kung'arisha uso
    Ndizi huwa na Vitamin C ambayo husaidia kuiweka ngozi kuonekana iking'aa. Kwenye ndizi iliyopondwa, ongeza vijiko viwili vidogo vya juisi ya limau na upake kwa uso na shingo. Osha kwa maji ya fufutende baada ya dakika 20. Ni vizuri kupaka mchanganyiko huu wakati unapoenda kulala.
    Kuzuia mikunjo
    Ponda parachichi na ndizi pamoja. Paka kwa uso na uoshe baada ya muda. Mchanganyiko huu hulainisha ngozi ya uso na kuwa laini lakini pia upunguza ukubwa wa matundu ya ngozi ya uso wako.
    Kusugulia uso (Scrubing)
    Changanya ndizi na sukari kijiko kimoja, kisha paka usoni na usugue taratibu. Ndizi hulainisha ngozi kavu na sukari huondoa seli zilizokufa kwenye ngozi.
    Saga ndizi moja na Oats vijiko vitatu kisha changanya na asali na maziwa. Paka usoni kwa dakika 15 kisha sugua.

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     JINSI YA KUWA NA NGOZI YA USO YENYE MVUTO KWA NJIA YA ASILI 

      

    Usafi wa  uso ni moja ya mambo muhimu sana kwa mwanamke au mwanaume yeyote  yule ambaye anapenda kuwa nadhifu na mwenye mvuto. Kumbuka “reception  ndio kila kitu “. Unapokutana na mtu sura yako na mwonekano wa sura yako ndio kitu cha kwanza kinachomtambulisha kwamba wewe ni nani  na upo kwenye hali gani.
    Kuna njia nyingi za kuufanya uso wako uvutie na kupendeza. Leo tutaongelea zaidi jinsi ya kusafisha uso kwa njia ya asili.  Mie hupenda kutumia njia ya asili sababu ni rahisi kupata vifaa na ni nafuu . Pia mtu anaweza kufanya kwa mazingira yoyote yale. Na matumizi ya vitu vya asili kwenye mwili husaidia kupunguza sumu mwilini kwani kitumia vipodozi vyenye kemikali husababisha miili yetu kujaaa sumu.
    Njia ya asili ya kusafisha na kupendezesha mwili ninayokueleza leo inahitaji vitu vikuu vinne : asali, sukari, maziwa, na limao.
    Haijalishi aina gani ya ngozi unayo , njia hii ya asili inaweza kutumika kwa aina yoyote ile ya ngozi iwe ngozi yenye mafuta au ngozi kavu.
    Kiasi cha mahitaji yanayohitajika:

    • Kijiko kimoja cha asali
    • Kijiko kimoja cha sukari
    • Kijiko kimoja cha maziwa
    • Kijiko kimoja cha limao

    Utaratibu wa kusafisha uso
    Weka  mahitaji hapo juu kwenye chombo kilicho kisafi, changanya vitu vyako mpaka vilainike, viache kwa muda wa dk 10 ili viweze kuchanganyikana vizuri na  na sukari iweze kuyayuka vizuri.
    Baada ya mchanganyiko wako kuwa tayari  chukua kipande cha pamba kilicho kisafi tumia kupakia mchanganyiko wako usoni . Na kumbuka ni vizuri uso ukiwa mchafu  na upaswi kuosha uso alafu ufanye  zoezi hili.Baada ya kupaka mchanganyiko wako usoni  kaa kwa dk 15 .
    Baada ya hapo chukua maji ya uvuguvugu, kitaulo kisafi na sabuni ya kipande “vizuri kutumia sabuni ya kipande maana haina kemikali nyingi” tumia kitambaa  kuoshea uso wako pamoja na sabuni.
    Basi baada ya hapo umekuwa umemaliza zoezi lako la usafi wa ngozi yako

    Kumbuka njia hii aina madhala yoyote na haibadilishi rangi au muonekano wa ngozi yako na unashauliwa kufanya mara kwa mara  ili kukupa mvuto zaidi.
      
    EPUKA NYWELE ZINAZOKATIKA KWA KUTUMIA KITUNGUU MAJI 
     
    Kitunguu maji kina sulphur ambayo husaidia kutengeneza  tishu za collagen katika mwili ambapo collagen husaidia kunurisha nywele na ngozi. Hivyo tunaweza kusema kuwa kitunguu maji husaidia kukuza nywele na kwa wale wenye nywele za kukatika, kupaka kitunguu maji mara kwa mara kinaweza kusaidia kupambana na tatizo hilo.
    Je utatumiaje kitunguu ili ufaidike na kitunguu maji kwa nywele zako. Soma zaidi hapa chini.
    Jinsi ya kuandaa
    • Chukua kitunguu kimoja au viwili kutegemeana na ukubwa wa kitunguu chenyewe. Fuata hatua zifuatazo:
    • Osha vizuri kitunguu au vitunguu na kisha ukimenye au uvimenye
    • Kata kitunguu au vitunguu vipande vidogo vidogo ili iwe rahisi kusaga au kutwanga
    • Saga kwenye brenda au twanga kwenye kinu , njia yoyote ile ambayo kwako ni rahisi kwako.  Visage au vitwange mpaka vilainike kabisa ili uweze  kutoa maji kwa urahisi.
    • Ukishasaga au kutangwa vitunguu , vichuje  vizuri ili upate maji maji .Zingatia usiweke maji kwa hivi vitunguu.
    Jinsi ya kupaka
    Nywele sio lazima ziwe safi maana  unapaswa  kuziosha  baada ya kupaka maji ya vitunguu.
    • Chukua pamba ambayo utatumia kupaka hayo maji ya vitunguu kwenye nywele zako. Paka zile sehemu ambazo nywele zimekatika. Unaweza pia paka  kichwa kizima.
    • Baada ya kupaka  unapaswa kuvaa kofia ya plastic na kitambaa kwa juu ili kuweza kupata joto . Tahadhali usikae kwenye mashine ya steam au dryer.
    • Ukiwa na kofia ya plastic na kitambaa kwa juu ya nywele zako , ukae hivyo hivyo kwa masaa  manne hadi matano.
    • Baada ya hapo unaweza kuosha na kukausha nywele zako na kuweka style yoyote ile.
    Hitimisho
    Ni vema kufanya zoezi hili la kupaka vitunguu walau mara mbili kwa mwezi. Ikiwa harufu ya kitunguu ni kali, unaweza weka asali kidogo kwenye maji ya vitunguu.
    Kwa matokeo mazuri  ya kukuza na kutunza nywele zako tumia vitunguu vidogo kufanya zoezi nililoeleza hapo juu.
     

     Njia Sahihi Ya Asili Ya Kukuza Nywele Zako

    Njia Sahihi Ya  Asili Ya Kukuza Nywele Zako

     1.Zifahamu aina ya  nywele zako

    kitu cha kwanza kujua ni kizifahamu nywele zako, kuna watu wanakaa na nywele bila kujua nwele zake ni za iana gani,Jinsi ya kujua aina ya nywele zako , chomoa nywele moja katika kichwa chako na uhakikishe imetoka na kale kamzizi kanakokuwa na rangi ya weupe ivi, kisha dumbukiza unywele huo kwenye glasi yenye maji na angalia kama unywele uo unaleta matokeo gani,kama itazama mara moja na haitanyanyuka tena basi jua nywele yako inanyonya unyevu kwa haraka ivyo inaitaji kuwa na unyevu unyevu na kama .
    Loading...
    2.Linda umyevu wa nywele zako.
    kama ilivyo kiu kwa binadamu, ndivyo hivyo nywele huitaji maji, kwaio kipindi unapokuwa unaosha nywele zako kabla ya kuzipaka mafuta ya kulinda nywele zako jitahidi kuwa una fanya  deep condition ili kuzifanya zibaki na unyevu .

    3.Usafi wa ngozi na nywele zenyewe pia.
    Kuna watu wanasema kuwa nywele zikioshwa mara kwa mara zinadumaa, lakini ulishawahi kujiuza endapo wewe utakaa bila kuoga.Nywele zinahitajika kuwa safi na ngozi yake pia ili kuifanya ngozi kufunguka na sio kufungwana ule uchafu wa mafuta.Matundu yanapokuwa wazi ndio ufanya nywele kuweza kujitokeza ivyo jitahidi kuosha nwele na kuhakikisha kuwa ngozi yako ni safi.

    4. Chagua Mafuta  bora ya kupaka
    Jitahidi kuchagua mafuta mazuri kwa ajili ya nywele zako.sio kila mafuta yanafaa kupaka katika nywele zako ingawa mafuta ya nazi ni mazuri zaidi au mafuta ya olive.kitu kizuri ni kuzijua nywele zako kwanza ndipo utaweza kujua pia bidhaa bora ya mafuta kwa ajili ya nywele.Ukishindwa ni bora kuonana na wataalamu wa mambo ya urembo.

    5.Epuka kuzisumbua nywele kila wakati.
    Ni vizuri kuwa unachana nywele kwa muoekano mzuri wa sura yako na nwele pia, lakini kitendo icho ufanya nywele kuwa zinapuputika sana,jitahidi kuwa unazisuka ili kuzifanya zikue pia.Kuchana chana nywel ni kuzisumbua.
    Inawezekana inakuwa ni ngumu kutambua nywele zake zinahitaji mafuta ya aina gani, au bidhaa gani ni bora zaidi kwa nywele zako, ni vizuri pia kuonana na wataalamu ili kuzisaidia nywele zako.

     JINSI YA KUKUZA NYWELE KWA KASI, NDANI YA MWEZI MMOJA


    Kila baada ya siku nne uwe na utaratibu wa kupakaa mchanganyiko wa hina na mayai, iwe na paste nzito kiasi, upake katika mizizi ya nywele, ukimaliza kupaka nywele zifunike kwa mfuko maalum ili zipate joto kwa muda wa masaa mawili, baada ya hapo zioshe kwa maji na shampoo, lakini maji yawe ya baridi yasiwe ya motooo au vuguvugu, yani yawe maji ya kawaida. Baada ya kuziosha zikaushe kwa taulo.


    NB: Nywele hazichanwi zikiwa na maji zimerowa kwani zitasababisha kung'oka kwa nywele na kusababisha upunguf wa nywele. Nywele zikishakauka. Paka mafuta ya nazi, au your favourate muhimu upake katika mizizi ya kichwa.

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     Na wakati unapaka mafuta kichwani kichwa kiinamishe chini, kiangalie chini ndio upake mafuta kichwa chako husaidia msukumo wa damu kufikia katika kichwa vizuri na kupata stimulation kwa kutumia ncha za vidole huku ukifanya massage kichwa taratibu kwa mda wa dakika tano, ukimaliza anza kuzichana taratibuu mpaka zilainike na uzibane..

     

     NB: Jaribu kwa siku uchane nywele mara mbili asbuh na jion, na nywele muda wote ziwe zenye mafuta. jizoeshe kufanyia massage kichwa chako kila wakati unaopaka mafuta kichwani. Uhai wa nywele ni mafuta kama ilivyo uhai wa binadamu utakuepo iwapo kuna maji.

     Namna bora ya kutunza kucha na kuepuka maradhi shambulizi ya kucha.

    Mikono, viganja na vidole ni kati ya sehemu muhimu katika mwili wa msichana. Mikono hutumika kufanya shughuli nyingi za nyumbani, shuleni na sehemu mbalimbali katika maisha kuanzia kutandika kitanda, kupika, kufanya usafi, kuandika, kujiremba pamoja na majukumu mengine mengi.

    Mikono isipotunzwa vizuri ni rahisi sana kuharibika, kupoteza mvuto wake wa asili na kuharibu afya ya kucha. Hitaji la urembo wakati mwingine humsukuma msichana katika matumizi ya vipodozi vya kupaka kwenye kucha zake ili kukamilisha urembo wake.

    Urembo wa vidole na kucha sio lazima ufanyike katika saluni au kwa wataalamu wa kupamba kucha, msichana anaweza kushughulikia afya na urembo wa vidole na kucha zake kwa gharama nafuu na kwa muda ambao mwenyewe anaona unafaa kufanya hivyo hata akiwa nyumbani.
    Hii pia itamsaidia Msichana kuchagua vipodozi salama kwa afya ya kucha zake na mwili kwa ujumla. Ni jambo la muhimu kufahamu kuwa baadhi ya vipodozi vinavyotumika katika urembo wa kucha, vina rangi na sumu zisizofaa kwa afya. Sumu kama vile ‘Formaldehyde na Toluene’ zinazopatikana katika baadhi ya rangi za kucha zina madhara kwa afya ya msichana.

    UR.jpg 
    Ni kweli kuwa kucha nzuri huongeza urembo, mvuto na furaha ya msichana lakini pia ni busara kukumbuka kuwa afya ni muhimu kuliko urembo na uzuri. Afya ya mwili na kucha za msichana kwa ujumla hutegemea chakula bora chenye protein, madini na vitamini na siyo rangi na vipodozi.

    Upungufu wa vitamini A, B Complex, proteni, madini ya chuma na chokaa (kalishiamu) mwilini husababisha kucha zipoteze afya yake ya asili. Kucha ambazo hazina afya zinaweza kuoza, kukauka, kupinda, kupasuka au kuwa na umbo kama kijiko. Magonjwa ya kuvu (fungus), na baadhi ya dawa za kupunguza makali ya virusi pia huharibu afya ya kucha. Mojawapo ya athari za dawa za kupunguza makali ya VVU aina ya Zidovudine (ZDV) ni kucha kuwa na rangi nyeusi.

    Kwa ajili ya afya bora ya kucha msichana anashauriwa kula mboga za majani, maharage, korosho, asali na matunda kwa wingi kila siku. Usafi wa kucha kila siku kwa kuziosha kwa maji ya uvuguvugu na sabuni laini pamoja na brashi ndogo ya mikono huimarisha afya ya kucha. Kucha pia zinaweza kusafishwa kwa maji ya mmea wa mshubiri (Aloevera), kitunguu saumu kilichopondwa pondwa au kitunguu maji kisha viganja na vidole vikaushwe vizuri na kupaka losheni.
    Image result for jinsi ya kutengeneza kucha bandia

    Kucha za msichana zinatakiwa zisiwe ndefu ili kuepuka utunzaji wa vimelea vinavyosababisha magonjwa na kurahisisha utunzaji na usafi wa kucha. Kucha ndefu zinaweza kuwa chanzo cha hatari kwa afya ya msichana na familia yake hasa pale msichana anapohusika na uandaaji wa chakula cha familia. Katika familia nyingi, hasa familia za kiafrika wasichana ndio wanaobeba wajibu na majukumu ya kuandaa chakula cha familia.

    Kwa afya nzuri ya kucha, msichana anashauriwa kukata kucha zake ili ziwe fupi kadri anavyotaka kwa kutumia ‘nail cutter’ au mkasi mdogo au wembe mpya ambao haujatumiwa na mtu mwingine. Kuchangia nyembe za kukatia kucha si salama kwani kunaweza kuwa njia mojawapo ya kusambaza vimelea vya magonjwa hatari ya kuambukiza kama vile virusi vinavyosababisha UKIMWI na ugonjwa wa homa ya ini.

    Image result for jinsi ya kutengeneza kucha bandiaNi vizuri kulainisha ncha za kucha baada ya kuzikata kwa kutumia tupa ya kucha (nail file) na kuzisugua kuelekea upande mmoja ili kuepuka kucha zisivunjike au zisisababishe michubuko ya ngozi wakati wa kujikuna. Kusugua kucha kwa kwenda mbele na nyuma kunaweza kusababisha kucha zivunjike kwa urahisi na haraka.

    Kwa afya njema ya kucha, msichana pia anashauriwa asifungue pini za barua au kukwangua vocha za simu kwa kutumia kucha. Kucha zisikatwe kwa kutumia meno na zisilowekwe kwenye maji kwa muda mrefu hasa pale maji hayo yanapokuwa na kemikali au sabuni.

    Kwa ajili ya afya njema ya kucha za miguuni, ni muhimu kuhakikisha kuwa, viatu kabla ya kuvaliwa vinakuwa vikavu na safi kabisa. Viatu visipotumiwa pia vihifadhiwe sehemu kavu isiyo na vumbi, maji au unyevunyevu ili kuepusha visiwe makazi ya kuvu (fungus)


    wadada NA wamama wanaopenda mitindo ya nywele. Tazama mitindo mbalimbali ya nywele

    [​IMG][​IMG]
    [​IMG]









    [​IMG]
    [​IMG]

    [​IMG]tarou wake nyweleno11

    Hakuna maoni

    Post Top Ad

    ad728

    Post Bottom Ad

    ad728