Header Ads

ad728
  • Breaking News

    Kuwa tajiri kwa mtaji wa laki 2 na Nusu tu kupitia ufugaji wa kuku wa kienyeji. Tazama Hapa

     

    Mpendwa msomaji wetu, yawezekana umekuwa ukiwaza sana nini ufanye ili uweze kufanikiwa na kuondokana na adha za umaskini.  Kulalamika tu vyuma vimekaza haitakusaidia kitu kama hutaki kujiongeza ili uongeze kipato chako.

    Yako mambo mengi ya kufanya ili kujikwamua kiuchumi. Usitegemee mshahara wako tu. Mimi nataka kukufungua macho kwa jambo moja tu tena kwa uchache. Jambo hili anaweza kulifanya mwenye mtaji mkubwa au mdogo.
     

    Somo  ni dogo tu lakini naamini wapo watakaopata mafanikio makubwa sana.
     
    Unaweza kuanza kwa mtaji wa Mil.1 mpaka laki tano au hata chini ya hapo.

    Mfano. Unaweza kutumia Tsh 250,000 kununua kuku 25 kwa bei ya Tsh 10,000 kwa kuku mmoja (kadirio la juu) Majogoo watakuwa 5 kwa uwiano wa 1:4.

    Hii ina maana kuwa wakishaanza kutaga utakuwa na

    vifaranga 20 x 10 = 200 Watunze vizuri.

    Wale vifaranga tunakadiria kuwa majike watakuwa 150 ambao ndani ya miezi 3 au zaidi nao wataanza kutaga.

    Utakuwa na kuku 200 + 25( ulioanza nao) =225 ndani ya miezi 6. Miezi 6 inayofuata 225 - (majogoo 55) = 170 Hii ina maana kuwa 170 x 10= 1,700.

    Ndugu msomaji, hayo niliyotoa ni makadirio ya chini sana hivyo mpaka mwisho wa mwaka utakuwa na kuku zaidi ya 2000. 

    Mwaka utakaofuata utakuwa na kuku wangapi baada ya kuuza kuku baadhi  ili upate fedha ya kuwalisha ????

    Ukiuza kuku 1000, utabaki na kuku 1000, kati yao tuseme majike ni 750. Ndani ya Miaka 2 maanake ni  750(majike) x 10 = kuku 7500 (uza wengine upate pesa ya kutumia kuwalisha) . 

    Tuseme sasa utabakiwa na kuku jike  3000 x 10( jike moja ni mayai 10) = kuku 30,000. 

    Hao kuku 30,000  ukiwauza wote utapata; 30,000x 13000( bei ya kawaida kbsa)= 390,000,000. Je, bado utakuwa masikini? Bado vyuma vitakuwa vimekaza?

    Nina uhakika, mpaka mwisho wa mwaka huo wa pili utakuwa umefanikiwa sana kuukimbia UMASIKINI.

    Kwenye hayo mamilioni, hata ukitoa milioni 100 kwamba  tuseme ndo zimetuka kuendeshea mradi wako, bado utakuwa ni milionea tu. Kumbuka huu ni mwongozo tu, fanya utafiti na ufuatilie zaidi.

    NB: Ukiyapata hayo mamilioni ya pesa, kumbuka kutoa Zaka, sadaka na kusaidia masikini wasiojiweza ili ubarikiwe zaidi 


     

    Maoni 1 :

    Post Top Ad

    ad728

    Post Bottom Ad

    ad728