Header Ads

ad728
  • Breaking News

    Serikali Yaitaka Sekta Ya Fedha Iwe Imara na Ihakikishe Huduma Zake Zinawafikia Wananchi Wa Mijini Na Vijijini



    WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema sekta ya fedha inapaswa kuwa imara na kuhakikisha huduma zake zinawafikia wananchi wengi katika maeneo ya mijini na vijijini ili iweze kutoa mchango unaokusudiwa katika kuinua uchumi wa nchi na ustawi wa jamii. 

    Ameyasema hayo leo (Jumatatu, Juni 24, 2019) wakati alipofungua Ofisi Ndogo na Tawi la Benki ya Biashara ya TIB jijini Dodoma. Amesema ukuaji wa sekta ya huduma za kifedha ni muhimu sana katika kukuza uchumi na kupunguza umaskini.

    Waziri Mkuu amesema benki ndicho chombo kikuu cha kutolea huduma za kifedha kwa wananchi, hivyo, benki zinatakiwa kuzingatia mahitaji ya wananchi, kuwahamasisha na kuwaelimisha umuhimu wa kutumia benki. 
    Mkurugenzi huyo amesema mbali na kufanikiwa katika kukuza mtaji, pia benki hiyo imeweza kukuza amana za wateja kutoka sh. bilioni 110 mwaka 2015 mpaka sh. bilioni 338 mwezi Disemba 2018, sawa na ukuaji wa asilimia 207.

    “Mafanikio mengine yabenki ya TIB katika kipindi cha miaka minne ni pamoja na kuanza kutengeza faida angalau ya sh. bilioni 1.3 mwaka jana (2018), kutoa mchango stahiki katika Mfuko Mkuu wa Serikali kiasi cha sh. milioni 250.”

    Mkurugenzi huyo ameongeza kuwa benki hiyo imetoa mikopo na dhamana kwa taasisi za umma hadi kufikia shilingi bilioni 224.35 kwa kipindi kilichoishia Machi 2019, kulipa kodi Serikalini kiasi cha sh. bilioni 19.2 tangu benki ianzishwe na kutoa mikopo kwenye sekta ya viwanda jumla ya sh. bilioni 65.12.

    Hakuna maoni

    Post Top Ad

    ad728

    Post Bottom Ad

    ad728